Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 25 Water and Irrigation Wizara ya Maji 209 2019-05-10

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:-

Usanifu wa Mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Miji ya Bisega, Bariadi, Itilima, Meatu na Maswa umekamilika kwa kiasi kikubwa lakini utanufaisha watu wa Maswa Mjini na baadhi ya vijiji katika Jimbo la Maswa Mashariki na kuliacha Jimbo la Maswa Magharibi bila ya maji ya uhakika:-

Je, kwa nini Serikali isichukue maji kutoka mji wa Algudu ambako tayari maji yameshafika na umbali ni mfupi ili Wananchi wa Kata za Malampaka, Mataba, Nyabubunza, Badi, Shishiyu, Masela, Sengwa, Jija, Kadoto, Mwanghondoli, Mwabayamla, Isanga, Busagi na Buchambi waweze kunufaika?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali natekeleza mradi wa maji safi kutoka Ziwa Victoria kwenye Miji ya Busenga, Bariadi, Itilima, Mwanhuzi na Maswa na vijiji vilivyo kilometa 12 kutoka bomba kuu la maji. Serikali pia inatekeleza mradi wa maji safi kutoka Ziwa Victoria kwenda katika Miji ya Ngudu na vijiji vilivyo ndani ya kilometa 12 kutoka bomba kuu. Vijiji hivyo ni Runele, Ngatuli, Nyang’onge, Damhi na Chibuji. Mradi huu ulihusu ulazaji wa bomba kilometa 25 na sehemu nyingine ya bomba kuu ilitumika bomba la zamani la mrai wa visima uliojengwa miaka ya 70. Bomba hilo ni lenye kipenyo cha nchi nane na kulingana na usanifu halitoshi kupanua zaidi kwenda Malampaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikal kupitia programu ya maendeleo ya sekta ya maji imetekeleza miradi ya maji ya Malampaka, Sayusayu, Mwasayi, Njiapanda na Sangamwalugesha ambayo miradi hii imekamilika na wananchi wanapata maji safi na salama. Serikali pia imekamilisha usanifu na uandaaji wa wa makabrasha ya zabuni kwa miradi ya maji ya Mwabulindi, Mwamanege na Badi ambao utahudumia vijiji vitatu vya Muhiba Jihu na Badi yenyewe.