Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 193 2019-05-08

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO (K.n.y. MHE. ESTER A. BULAYA) aliuliza:-

TANESCO Mkoa wa Mara katika zoezi la kupeleka umeme vijijini walipitisha nguzo za umeme kwenye maeneo ya watu katika Kijiji cha Nyabeu, Kata ya Guta na uthamini ulifanyika na iliahidi malipo kufanyika lakini hadi leo hawajalipwa na badala yake wanaambiwa maeneo hayo ni ya TANESCO:-

(a) Je, ni lini Serikali itawalipa wananchi hao fidia stahiki?

(b) Je, ni kwa nini TANESCO inamiliki maeneo kabla ya kulipa fidia?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, miradi ya kupeleka umeme katika Wilaya za Serengeti, Bunda na Ukerewe ilitekelezwa kati ya mwaka 2003 na 2006 chini ya ufadhili za Serikali za Sweden na Hispania kupitia Mashirika yake ya Kimataifa ya Maendeleo SIDA na Spanish Funding Agency pamoja na Serikali ya Tanzania. Kazi ya tathmini ya mali za wananchi waliopisha mradi ilifanywa na Mtathmini Mkuu wa Serikali na malipo yalifanyika mwaka 2009. Ulipaji wa fidia hiyo ulifanyika kwa kuwashirikisha Watendaji wa Vijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa kuridhia orodha ya wananchi waliostahili kulipwa fidia hiyo. Jumla ya Sh.135,820,993 zililipwa kwa wananchi waliopisha mradi huo ikiwa ni pamoja na wananchi wa Kijiji cha Nyabeu.

Mheshimiwa Spika, TANESCO huchukua maeneo baada ya kufanya tathmini kupitia Mthamini Mkuu wa Serikali na kuwalipa wananchi wanaopisha ujenzi wa mradi.