Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 192 2019-05-08

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-

Jimbo la Tunduru Kusini lina jumla ya vijiji 65, kati ya hivyo ni vijiji vinne tu ndiyo vimefikiwa na umeme wa REA Awamu ya I na ya II:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika vijiji 61 vilivyobaki?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Idd Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Jimbo la Tunduru Kusini lina vijiji 65, kati ya vijiji hivyo Vijiji vinne vya Azimio, Chiwana, Mkandu na Mbesa ndivyo vimekwishapata umeme kupitia mradi wa REA II na Vijiji vingine vinne vya Mchuluka, Umoja, Masalau na Msinji vinatarajiwa kupatiwa umeme kupitia mradi wa REA III mzunguko wa kwanza unaoendelea na unaotegemea kukamilika mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Tunduru Kusini inahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilometa 9.4, ujenzi wa njia ya msongo wa umeme wa kilovolts 0.4 yenye urefu wa kilometa nane, ufungaji wa transfoma nne za KVA 50 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 275. Gharama za kupeleka umeme katika vijiji hivyo ni shilingi milioni 644.

Mheshimiwa Spoika, vijiji 57 vya Kata za Chiwana, Mchuluka, Mtina, Nalasi, Mchoteka, Ligoma, Tuwemacho na Lukumbulu vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya III, mzunguko wa pili unaotarajiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021. ahsante.