Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 176 2019-05-07

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Hospitali ya Wilaya ya Lushoto ni ya muda mrefu na hata ujenzi wa majengo yake ni wa kizamani ambao hauendani na utoaji huduma na Serikali ina utaratibu wa kukarabati na kuongeza majengo katika Hospitali za Wilaya:-

Je, ni lini Hospitali ya Wilaya ya Lushoto itakarabatiwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shaabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Lushoto ni miongoni mwa Hospitali Kongwe za Wilaya nchini na imekuwepo tangu mwaka 1967. Tangu kuanzishwa kwake, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleleo imefanya ukarabati na upanuzi wa majengo kama ifuatavyo:-

(i) Mwaka wa fedha 2006/2007, ujenzi wa jengo la mapokezi, jengo la wagonjwa wa nje, jengo la famasi, jengo la maabara na jengo la upasuaji kupitia mradi wa KfW;

(ii) Kwa mwaka wa fedha 2008/2009, ujenzi wa jengo la kuhifadhia maiti kwa maana ya mortuary na uwekaji wa vigae (tiles) katika wodi zote;

(iii) Kwa mwaka wa fedha 2011/2012, ujenzi wa jengo kwa ajili ya ndugu wa wagonjwa kusubiria yaani waiting bay;

(iv) Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, ukarabati mkubwa wa jengo la upasuaji;

(v) Kwa mwaka wa fedha 2016/2017, ukarabati wa jengo la mapokezi, jengo la wagonjwa wa nje, jengo la famasi, jengo la maabara, jengo la wodi ya watoto na ujenzi wa jengo la dawa za ziada la Halmashauri kwa maana ya buffer store;

(vi) Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, ujenzi wa kichomea taka (Incinerator) na shimo la kutupia kondo la nyuma la uzazi kwa maana ya placenta pit;

(vii) Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, ukarabati wa jengo la CTC linalovuja unaendelea kupitia ufadhili wa AMREF.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kukarabati miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini kwa kadri upatikanaji wa fedha utakavyokuwa unaruhusu.