Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 21 Water and Irrigation Wizara ya Maji 175 2019-05-06

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-

Miradi ya maji katika vijiji vya Lupunga, Ruvu Dosa na Kipandege Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha bado inasuasua mpaka sasa.

Je, ni lini miradi hiyo itapatiwa fedha ili iweze kukamilika?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji Lupunga uliopo Kata ya Kikongo ulianza kutekelezwa Novemba, 2013 na ulikamika mwaka 2016 na unaendelea kutoa huduma ya maji katika vitongoji tisa vya Ngeta, kikongo, Lupunga, Mwanabwito, Makongotopola, Kisabi, Madimula, Msongola na Makazi Mapya kwenye mamlaka ya mji mdogo wa Malandizi. Mradi huo ulikuwa na changamoto za kiundeshaji ambapo kamati ya Maji ya awali ilivunjwa na kuundwa kamati mpya inaendelea kutoa huduma ya maji maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji Ruvu kwa Dosa uliopo katika Kata ya Matambani ulianza kutekeleza mwaka 2013 na kukamilika mwaka 2016 kutoka bomba kuu la DAWASA. Kwa sasa mradi unaendelea kutoa huduma ya majisafi na salama kwa wananchi 1800 kwa eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Maji kipandege uliopo katika Kata ya Soga ulianza kutekelezwa Novemba, 2013 na kukamilika mwaka 2017. Mradi huo kwa sasa una changamoto za kiufundi ikiwa ni msukumo mdogo wa maji toka bomba la DAWASA. Tayari Mkandarasi na Mhandisi Mshauri aliyesanifu wanashukulikia tatizo hilo. Lengo la Serikali ni kuhakikisha miradi yote inatoa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa maeneo hao.