Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 168 2019-05-06

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-

Kumekuwa na baadhi ya Askari wa barabarani wanaosimamisha magari hasa yale ya safari ndefu wakitokea vichakani (kujificha) na hatimaye wakati mwingine kusababisha ajali:-

Je, ni Askari wangapi kama hawa wameshachukuliwa hatua za kinidhamu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi nchini chini ya Sheria ya Usalama Barabarani Sura 168 iliyorejewa mwaka 2002, inamtaka Askari wa Polisi kuhakikisha usalama wa watumiaji wote wa barabara. Katika kutekeleza hilo, Polisi wanatumia mbinu mbalimbali kwa mujibu wa sheria na taratibu ambazo zinawaongoza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lako Tukufu litakumbuka kuwa wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani kulikuwa na mfululizo wa ajali nyingi barabarani hususan zile ambazo zinahusisha magari ya abiria. Kwa kuzingatia hilo, Baraza la Usalama Barabarani lilibuni mkakati maalum uliofanikisha kupunguza ajali kwa asilimia 43 mpaka sasa. Mkakati huu ulihusisha mbinu mbalimbali zenye lengo la kuwalazimisha madereva kufuata sheria za usalama barabarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haina ushahidi wa matukio ya askari waliowahi kusababisha ajali barabarani kwa sababu ya kujificha. Hata hivyo, Serikali kupitia Baraza la Taifa la Usalama Barabarani limejiwekea utaratibu wa kufanya uchunguzi wa kina kwa kila ajali kubwa inayotokea na kuchukua hatua stahiki inapobainika kuna uzembe wa usimamizi wa sheria au uvunjifu wa Sheria za Usalama Barabarani.