Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 17 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 145 2019-04-29

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:-

Hivi karibuni Mheshimiwa Rais alitoa agizo la kutatua migogoro ya vijiji na hifadhi mbalimbali na orodha ya vijiji vyenye migogoro toka Jimbo la Nkasi imefikishwa na kupokelewa na Wizara:-

Je, ni lini migogoro ya vijiji vya Kasapa, King’ombe, Mlambo, China, Nkomanchindo na vinginevyo vilivyoondoshwa vitapatiwa ufumbuzi?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Desderius John Mipata, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mheshimiwa Mbunge anavyofahamu, utatuzi wa migogoro iliyopo katika vijiji vyote nchini na hifadhi vikiwemo vijiji Kisapa, King’ombe, Mlambo, China na Nkomanchindo umetolewa maelekezo na Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani yangu kwamba mara utekelezaji wa maelekezo hayo utakapokamilika, ufumbuzi wa migogoro hiyo utakuwa umepatikana. Nitoe rai kwa wananchi kuacha kuvamia maeneo mapya ya hifadhi wakati huu, wakati migogoro huo unasubiri yanatafutiwa ufumbuzi.