Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 141 2019-04-29

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA (K.n.y. MHE. SUSAN L. KIWANGA) aliuliza:-

Mji Mdogo wa Mlimba unazungukwa na Kata za Chisano, Kalengakelo na Kamwene na zina jumla ya wakazi wasioupungua elfu hamsini na nane ambapo hawana maji kwa matumizi ya nyumbani na kunywa; na kwa kuwa kuna chanzo kikubwa cha maji na Mhandisi wa Halmashauri ameshaleta andiko la mradi wa maji:-

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za mradi huo ili wananchi hao wapate maji ya kunywa safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto ya maji kutotosheleza wakazi wa Kata za Mlimba, Chisano, Kalengakelo na Kamwene waliopo katika Jimbo la Mlimba, Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kwa kushirikiana na Wizara ya Maji imesanifu mradi mkubwa wa maji ambao utahudumia wakazi zaidi ya 29,713. Mradi huu utakapokamilika utatatua kero ya maji katika kata zilizotajwa hapo juu ikiwemo Mlimba kwa kuondoa mgao wa maji kabisa.

Andiko la mradi huu linafanyiwa kazi na Wizara ya Maji ili Serikali iweze kutafuta fedha zaidi ya shilingi bilioni 4.5 kuweza kufanikisha ujenzi wa mradi huu ambao umeonekana kuwa suluhisho la maji katika Jimbo la Mlimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika jitihada hizo za kuwapatia wananchi wa Jimbo la Mlimba huduma ya maji safi na salama, Serikali kupitia program ya maji inaendelelea na ujenzi wa mradi wa maji wa Kata za Chita/ Ching’anda a Mbingu/Vigaeni. Pia imekamilisha ujenzi wa miradi ya maji saba katika Vijiji vya Tangamyika, Masagati, Matema, Kamwene, Viwanja Sitini, Mlimba A na B, Namwawala na Idete.