Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 137 2019-04-29

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JORAM I. HONGOLI aliuliza:-

Madeni ya Halmashauri hususan mikopo ya vijana na wanawake ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 2016 yamekuwa hayalipiki kutokana na Halmashauri nyingi kutokuwa na mapato ya kutosha kuendesha Halmashauri hizo hasa miradi ya maendeleo.

Je, ni kwa nini madeni hayo yasifutwe ili kuondoa hoja za ukaguzi kwenye Halmashauri hizo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joram Ismael Hongoli, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikitoa fedha za mikopo kwa ajili ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotokana na asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali. Katika kipindi chote cha utekelezaji hakukuwa na sheria kwa ajili ya kusimamia utengaji na utoaji fedha hizo na kusababisha kuwepo kwa changamoto mbalimbali ikiwemo malimbikizo ya fedha ambazo hazikutolewa kwa walengwa katika kipindi husika na kusababisha hoja za ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutungwa kwa Sheria ya Usimamizi wa Fedha hizo, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inakusudia kuyafuta malimbikizo hayo kama ilivyoelekezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kazi ya kuhakiki takwimu, kubaini kiasi ambacho kimelimbikizwa katika Halmashauri zote nchini inaendelea na Mara tu itakapokamilika, taratibu za kufuta malimbikizo hayo zitafanyika. Aidha, kwa sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI inazisimamia kwa karibu Halmashauri ili kuhakikisha zinatoa fedha hizo kwa mujibu wa Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.