Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 132 2019-04-25

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELSTER A. BURA aliuliza:-

Mkoa wa Dodoma una upungufu wa Walimu 527wa Sayansi:-

Je, ni lini Serikali italeta Walimu wa kutosha wa sayansi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Aloyce Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa Mkoa wa Dodoma una shule 221 za sekondari zikiwa na wanafunzi 72,254. Mahitaji ya Walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati ni Walimu 1,641 na Walimu waliopo ni 916, hivyo pungufu ni Walimu 527 sawa na asilimia 32 ya mahitaji halisi.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri Walimu wa masomo hayo kwa awamu na kwa sasa kibali cha kuajiri Walimu 4,549 kimetolewa ambapo kati ya hao Walimu 1,374 ni wa masomo ya Sayansi na Hisabati. Taratibu za kuajiri Walimu hao zinakamilishwa ili kuwapanga Walimu hao katika Halmashauri zenye upungufu ikiwepo Halmashauri za Mkoa wa Dodoma. Ahsante.