Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 114 2019-04-23

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. UPENDO F. PENEZA) aliuliza:-

Je, katika mwaka 2016/2017 na 2017/2018 Serikali ilikusanya kiasi gani cha kodi ya 18% (VAT) kwa taulo za kike (sanitary pads) zote zilizotengenezwa nchini na zile zilizoingizwa nchini kabla ya kodi hiyo kuondolewa?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Upendo Furaha Peneza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/ 2017, Serikali ilikusanya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya kiasi cha shilingi bilioni 3.01 na shilingi bilioni 2.54 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwenye bidhaa ya taulo za kike zilizoingizwa nchini pamoja na zile zilizozalishwa hapa nchini kabla ya kodi hii kuondolewa Juni, 2018.