Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 113 2019-04-23

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO aliuliza:-

Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Songwe yapo Mbozi na hakuna barabara ya kuunganisha Wilaya mpya ya Songwe kufika mkoani hadi upitie Mbeya:-

Je, Serikali haioni haja ya kutengeneza barabara ya mkato toka Songwe kupitia Kata ya Magamba kwenda Mbozi Makao Makuu ya Mkoa ili kuwarahisishia usafiri wananchi wa Wilaya ya Songwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Phillipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishaona haja ya kutengeneza barabara ya mkato kutoka Wilaya ya Songwe kwenda Wilaya ya Mbozi kupitia Kata ya Magamba. Barabara iliyopendekezwa inaitwa Galula – Itindi – Magamba yenye urefu wa kilometa 32.

Mheshimiwa Spika, barabara hii imeshaanza kutengenezwa kupitia TARURA ambayo katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 imetengwa shilingi milioni 65 kwa ajili ya kujenga daraja lenye urefu wa mita tisa katika Kijiji cha Itindi na mpaka sasa Mkandarasi anaendelea na kazi. Vilevile katika mwaka wa fedha 2019/2020, barabara hii imeombewa kiasi cha shilingi milioni 63 kwa ajili ya kufanya matengenezo sehemu korofi kwa urefu wa kilometa saba.

Mheshimiwa Spika, TARURA Wilaya ya Songwe inaendelea kufanya usanifu wa kina ili kujua mahitaji na gharama halisi za kufanyia matengenezo makubwa. Mara kazi hiyo itakapokamilika Serikali itatafuta fedha kuhakikisha inajenga barabara hiyo na kufanya ipitike majira yote ya mwaka.