Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 89 2019-04-16

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-

Wananchi wa Kata za Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea Liwiti, Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata wamekuwa wakitumia fedha na muda mwingi kwenda kutafuta bidhaa na huduma katika masoko ya Buguruni na Kariakoo kutokana na kukosa huduma hizo katika maeneo yao:-

(a) Je, kwa nini Serikali isijenge soko kubwa katika eneo mbadala lililo katikati na linaloweza kufikiwa na wananchi hao kwa wakati?

(b) Je, kwa nini Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017 lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaozunguka soko hilo na maeneo ya karibu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli, Mbunge wa Segerea, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala iliweka kipaumbele cha kutekeleza mradi wa kimkakati wa ujenzi wa Soko la Kisutu utakaogharimu takribani shilingi bilioni 12.17. Mpaka sasa mradi huo umepatiwa jumla ya shilingi bilioni 3.92 na ujenzi unaendelea. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya kujenga masoko mengine ndani ya Manispaa ya Ilala. Halmashauri inashauriwa kutumia fursa ya miradi ya kimkakati na kuandaa andiko la mradi wa kujenga masoko katika Kata ya Kinyerezi, Bonyokwa, Segerea, Liwiti Kipawa, Kimanga, Kisukulu na Tabata ili kupata fedha za utekelezaji.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 limepangwa kuanza kutumika Mei, 2019 baada ya matengenezo ya choo ambacho kilikuwa hakijakamilika kwa wakati huo.