Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 10 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 83 2019-04-15

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:-

Je, ni lini Kituo cha Misugusugu “Check Point” kitahamishwa, kwani kimekuwa kero kutokana na vumbi linalosababishwa na miundombinu mibovu?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mradi wa kituo cha pamoja cha ukaguzi wa mizigo (One Stop Inspection Station) ili kuziwezesha mamlaka za ukaguzi wa mizigo kufanya kazi ya ukaguzi katika eneo moja. Mradi huu unatekelezwa sambamba na mradi wa mizani ya ukaguzi wa mizigo iliyopo Vigwaza Mkoa wa Pwani. Taasisi zinazohusika katika mradi huu ni pamoja na TANROADS, Polisi na Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya Mapato Tanzania ipo katika hatua za awali za kujenga na kusimika mifumo ya ukaguzi katika eneo la mradi lililopo Vigwaza, hivyo basi kituo cha ukaguzi wa mizigo kitahamishiwa kutoka Misugusugu kwenda vigwaza mara baada ya kazi ya kujenga na kusimika mifumo itakapokamilika.