Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 75 2019-04-12

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-

Katika Jimbo la Mpwapwa Vijiji vya Mkanana, Nalamilo, Kiboriani, Igoji Kaskazini, Mbori, Tambi, Nana, Majani (Mwenzele), Mafuto, Kiegea, Kazania, Chimaligo, Mbugani, Chilembe, Mazaza, Mwanjili, (Makutupora) na Chibwegele havina huduma ya umeme:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia huduma ya umeme vijiji hivyo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya vijiji 31 katika Wilaya ya Mpwapwa vitapatiwa umeme kupitia Miradi ya Umeme Vijijini inayoendelea. Kupitia Mradi wa REA III Mzunguko wa Kwanza unaoendelea jumla ya vijiji 14 vitapatiwa umeme. Hadi sasa Vijiji vya Mbori, Tambi, Mnase, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mpwapwa, Kimangai na Chunyu Sekondari vimepatiwa umeme kupitia Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA III) Mzunguko wa Kwanza unaoendelea kutekelezwa hivi sasa na mkandarasi Kampuni ya A2Z Ifra Engineering Limited kutoka nchini India. Kazi za mradi katika Wilaya ya Mpwapwa zinahusisha ujenzi wa njia za umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 9.45, njia za umeme wa msongo kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 68, ufungaji wa transfoma 34 za kVA 50 na 100, pamoja na kuunganisha umeme kwa wateja wa awali 1,148 na gharama za mradi ni shilingi bilioni 2 na milioni 600.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyosalia ikiwa ni pamoja na Mkanana, Ngalamilo, Kiboriani, Nana, Majami, Mafuto, Kiegea, Kazania, Chimaligo, Mbugani, chihembe, Mazaza, Mwanjiri na Chibwegerea vitapatiwa umeme katika Mzunguko wa Pili wa Mradi wa REA III unaotarajiwa kuanza Julai, 2019 na kukamilika Juni, 2021. Ahsante.