Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 66 2019-04-11

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:-

Gesi ambayo imegunduliwa katika Mkoa wa Mtwara itanufaisha wananchi wote nchini na Taifa kwa ujumla:-

Je, Serikali ina mpango gani mahususi wa kujenga Chuo kitakachotoa mafunzo ya gesi na mafuta katika Kanda ya Kusini ili vijana wa Lindi na Mtwara na maeneo mengine waweze kupata taaluma na kuweza kushiriki kwenye sekta hii?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Aziz Mtamba, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali itaendelea kuvitumia vyuo vilivyopo nchini kuwajengea uwezo wa kitaaluma wananchi katika masuala ya utafutaji, uendelezaji, uzalishaji, uchakataji, usafirishaji na usambazaji wa mafuta na gesi asilia. Kwa mfano, kwa mwaka 2010 Kampuni ya Petrobras ilitumia Dola za Marekani 350,000 sawa na shilingi milioni 780 kufundisha na kukipatia Chuo cha VETA Mtwara vifaa vya mafunzo. Aidha, kupitia mpango huo wanafunzi 50 na wakufunzi wawili walifundishwa kwenye fani ya umeme na makanika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Statoil imekuwa ikifadhili mafunzo mbalimbali kwa ngazi za vyuo kwa mfano mwaka 2013 ilifadhili wananchi tisa kusoma shule ya biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, masuala ya fedha na uchumi wamafuta na gesi asilia. Aidha, Kampuni ya BG waliendesha mafunzo na VETA Mtwara kwenye fani za English Language, Food preparation, Plumbing, Welding, Carpentry, Motor Vehicle Maintenance, Electrical Installation and Maintenance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia iliyokuwa Wizara ya Nishati na Madini mwaka 2013 ilitoa ufadhili kwa wanafunzi 50 kusoma Chuo cha VETA Mtwara. Aidha, Serikali kupitia TPDC imefungua klabu 32 za mafuta na gesi katika shule za sekondari za mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kutoa elimu inayohusu tasnia ya mafuta na gesi asilia pamoja namna inavyoweza kuwanufaisha kupitia fursa zinazotengenezwa na tasnia hii katika maeneo yao.