Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 63 2019-04-11

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:-

Mto Kagera ni chanzo muhimu kinachoweza kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wanaopakana nao:-

Je, kwanini Serikali isifanye utaratibu wa kuvuta maji hayo ili yawasaidie wakazi wa maeneo hayo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Diodorus Buberwa Kamala, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshaanza mipango ya kutumia Mto Kagera kama chanzo cha maji katika maeneo mbalimbali yanayopakana na Mto huo. Kwa sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bukoba (BUWASA) imepanga kuutumia Mto Kagera kama chanzo cha maji kwa Miji ya Kyaka na Bunazi pamoja na vijiji mbalimbali vinavyozungukwa na mto huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji wa mradi kwenda Miji ya Kyaka na Bunazi kwa kutumia chanzo cha mto huo, BUWASA imemwajiri mtaalam mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu na uandaaji wa makabrasha ya zabuni na matarajio ya usanifu huo utakamilika mwezi Septemba, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matarajio ya ujenzi wa mradi huo utaanza katika mwaka wa fedha 2020/2021.