Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 57 2019-04-10

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA (K.n.y. MHE. PETER A. LIJUALIKALI) aliuliza:-

Je, ni lini programu ya REA III itaanza kutekelezwa katika vijiji ndani ya Wilaya ya Kilombero?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Peter Ambrose Lijualikali, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ilianza kutekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini ikiwemo vijiji vya Wilaya ya Kilombero Julai, 2018.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kampuni ya State Grid Electrical and Technical Works Ltd Novemba, 2018 ilikamilisha upimaji na usanifu katika vijiji 21 vya REA III, Mzunguko wa Kwanza. Kwa sasa mkandarasi anaendelea na kazi ya ujenzi wa miundombinu katika Vijiji vya Kirama, Mbasa, Michenga, Mautanga, Ihanga na Miwangani. Kazi za ujenzi wa mradi huu zitakamilka mwezi Juni, 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za mradi wa Jimbo la Kilombero zinahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa Kilovoti 33 umbali wa kilomita 16.5, njia ya umeme wa msongo wa Kilovoti 04 urefu wa kilomita 28, ufungaji wa transformer 14 za KVA 50 na 100, pamoja na kuunganisha umeme wateja wa awali 497 na gharama ya mradi ni shilingi 1,700,060,000/=. Ahsante sana.