Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 55 2019-04-10

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI aliuliza:-

Mara ni mkoa ambao una makundi makubwa ya jamii ya wafugaji, wakulima na wavuvi lakini kwa sasa kuna shida kubwa ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji:-

Je, ni lini wafugaji watapatiwa eneo kwa ajili ya kuendesha shughuli zao?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joyce Bitta Sokombi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mara unakadiriwa kuwa na ng’ombe 1,305,075, mbuzi 733,321, kondoo 437,387,
nguruwe 5,802, punda 11,757 na kuku 1,524,653. Upande wa Nyanda za Juu katika Wilaya za Serengeti, Tarime, Rorya, Butiama na Bunda ndizo zenye ufugaji mkubwa wa mifugo ambapo Wilaya za Musoma, Rorya na Bunda kwa kiasi kikubwa zinashughulika na uvuvi hasa kwenye vijiji vya mwambao wa Ziwa Viktoria.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mara kupitia Halmashauri 9 umeshatenga maeneo yenye jumla ya ukubwa wa hekta 15,588.55 kwa ajili ya malisho ya mifugo kupitia mpango wa matumizi ya ardhi ya vijiji. Mkoa kupitia Halmashauri utaendelea kutekeleza mpango wa matumizi ya ardhi kwa vijiji ili kuainisha matumizi ya ardhi kwa makundi mbalimbali wakiwemo wafugaji na wakulima ili kuepusha migogoro. Ahsante.