Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Madini 52 2019-04-09

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-

Wananchi wa Kijiji cha Busiri, Wilayani Biharamulo ni miongoni mwa Watanzania ambao wanaendesha maisha kwa shughuli za uchimbaji mdogo kama ilivyo kwa wenzao wengi na kwingineko nchini. Uchimbaji mdogo wa Busiri unahitaji kuungwa mkono na Serikali kimkakati:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaunga mkono wachimbaji wadogo wa Busiri na ni upi?

(b) Je, Serikali ipo tayari kuwatembelea wananchi wa Kijiji cha Busiri ili kuwaelewesha ni namna gani itaanza utekelezaji wa mpango huo wa kuwaunga mkono wachimbaji hao?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, lenye vipengele
(a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ina mikakati mingi ya kuwaunga mkono wachimbaji wadogo nchini wakiwemo wachimbaji wa Kijiji cha Busiri, Wilaya ya Biharamulo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mkakati wa kuwasadia wachimbaji wadogo nchini kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limenunua mtambo mkubwa wa kusaidia kufanya utafiti wa kina kwa kuchoronga miamba kwa bei nafuu ili kubaini mashapo zaidi na hivyo kuongeza uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini inakamilisha uandaaji wa kitabu cha madini yapatikanayo Tanzania, toleo la nne, ambacho kinaonesha uwepo wa madini katika mikoa, wilaya, vijiji, hivyo kusaidia wananchi na wachimbaji wadogo ikiwemo wa Kijiji cha Busiri kutambua madini yaliyopo katika maeneo yao na matumizi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali za Madini (SMMRP), inakamilisha kujenga vituo vya umahiri katika Wilaya za Bukoba, Bariadi, Songea, Handeni, Musoma, Mpanda na Chunya ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kujifunza kwa vitendo. Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara kwa wachimbaji wadogo ili wanufaike zaidi na kazi ya uchimbaji.