Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 34 2019-04-08

Name

Lameck Okambo Airo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-

Wakati wa ziara ya Kampeni za Uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga daraja la kuunganisha Tarafa tatu za Luoimbo, Suba na Nyancha na tayari Halmashauri imeshapeleka makadirio Wizarani:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lameck Okambo Airo, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, daraja linalounganisha Tarafa za Luoimbo, Suba na Nyancha ni miongoni mwa ahadi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizozitoa maeneo mbalimbali nchini wakati wa Kampeni ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umefanya tathmini ya gharama za ujenzi huo na wamepata kiasi cha shilingi bilioni 1.15. Serikali inaendelea na jitihada za kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa daraja hilo. Azma ya Serikali ni kuhakikisha ahadi hiyo pamoja na ahadi nyingine zilizotolewa na viongozi wakuu wa kitaifa zinatekelezwa ndani ya kipindi cha miaka mitao ijayo. Ahsante.