Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 25 2019-04-05

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:-

Serikali inajitahidi sana kukabiliana na tatizo la maji katika Manispaa ya Morogoro, lakini tatizo hilo lipo kwenye baadhi ya Kata:-

Je, Serikali ina mikakati gani ya makusudi ya kumaliza tatizo hili katika Manispaa ya Morogoro?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) inaendelea na uboreshaji wa huduma ya maji katika Manispaa ya Morogoro kwa mipango ya muda mfupi na muda mrefu. Katika mipango ya muda mfupi, katika mwaka wa fedha 2018/2019, MORUWASA imetekeleza mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji katika Kata za Kihonda na Mkundi. Mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.9 na umewanufaisha wakazi wapatao 17,000 wanaoishi maeneo ya Kihonda Kilimanjaro, Yespa, Kiegea na Kihonda Kaskazini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mpango wa muda mrefu, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika la Maendeleo la AFD itatekeleza mradi wa kuboresha huduma ya majisafi katika Manispaa ya Morogoro. Kazi zitakazotekelezwa ni kuongeza kina cha bwawa la Mindu, ujenzi wa mtambo wenye uwezo wa kusafisha na kutibu maji, upanuzi wa mtambo wa kusambaza maji, ukarabati wa mabwawa ya majitaka kwa gharama ya Euro milioni 70. Kwa sasa Wizara inasubiri kusainiwa kwa mkataba wa kifedha kati ya Wizara ya Fedha na Shirika la Maendeleo la Ufaransa la AFD kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.