Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 20 2019-04-04

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:-

Pamoja na mambo mengine, Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano imelenga kuongeza asilimia za upatikanaji wa maji vijijini.

(a) Je, lini Serikali itafanya utafiti wa vyanzo vya maji katika Jimbo la Mkalama ili kuwa na uhakika wa rasilimali hiyo?

(b) Je, lini Serikali itatoa fedha za kutosha kuwapatia maji safi wananchi wa Jimbo la Mkalama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Allan Joseph Kiula, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, lenye kipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/ 2019, Serikali kupitia Wizara ya Maji imetenga kiasi cha shilingi milioni 450 kwa ajili ya kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi katika maeneo kame ya Mikoa ya Singida, Mwanza, Tabora na Shinyanga. Utafiti huo utahusisha pia Wilaya ya Mkalama ambapo shilingi milioni 50 zitatumia.

Mheshimiwa Spika, pamoja na utafiti unaotarajiwa kufanyika, Serikali imekua ikitekeleza miradi mbalimbali yamaji katika Vijiji vya Ndunguti, Kinyangiri, Ipuli na pia inatekeleza miradi ya uchimbaji wa visima 24 katika maeneo mengine tofauti. Ili kuhakikisha miradi hii inakamilika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 1.36 kwa mwaka wa fedha 2018/2019.