Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 19 2019-04-04

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:-

Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa hupata posho shilingi elfu ishirini kwa mwezi kiasi ambacho ni kidogo ikilinganishwa na kazi kubwa wanayoifanya:-

Je, ni lini Serikali itaongeza posho kwa Wenyeviti hao?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS – TAMISEMI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alfredina Apolinary Kahigi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wenyeviti wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji katika shughuli za maendeleo. Hata hivyo, kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Mitaa, vitongoji na Wajumbe wa Serikali za Vijiji pamoja na Wajumbe wa Mitaa za mwaka 2014 zilizotolewa kupitia Tangazo la Serikali Na. 322 na Na. 323, sifa zinazomwezesha mkazi wa
Mtaa, Kijiji na Kitongoji kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti au mjumbe wa Serikali za Mitaa ni pamoja na kuwa na shughuli halali inayomwingizia kipato.

Mheshimiwa Spika, Serikali inalipa posho ya Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa kwa kutumia asilimia 20 ya mapato ya ndani inayorejeshwa na Halmashauri kwenye ngazi za Serikali za Mitaa. Hata hivyo, kiasi hicho kinategemea hali ya makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri yanayokusanywa kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290. Mkakati uliopo ni kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuimarisha makusanyo katika vyanzo vya mapato vilivyopo kwa kutumia mifumo ya kielektroniki ili kujenga uwezo wa kulipa posho kwa viongozi hao. Aidha, viwango vya posho inayolipwa vinatofautiana kati ya Halmashauri moja na nyingine kulingana na uwezo wa kifedha uliopo.