Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 14 2019-04-03

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Gereza katika Wilaya ya Chunya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hadi sasa nchini kuna Wilaya 51 ambazo hazina Magereza ya Wilaya ikiwemo ya Chunya. Hata hivyo, lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa kila Wilaya inakuwa na Gereza ili kuwahifadhi wahalifu wa Wilaya husika, kwani uwepo wa Gereza kwenye kila Wilaya utapunguza gharama za kuwasafirisha wahalifu kutoka Wilaya moja na kuharakisha uendeshwaji kesi sambamba na kupunguza msongamano wa mahabusu.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali inaendelea na mpango wa ujenzi wa magereza kwa awamu kwenye Wilaya zisizokuwa na magereza. Hata hivyo, kasi ya ujenzi huo imekuwa ni ndogo kutokana na kuathiriwa na uhaba wa rasilimali fedha. Hivyo Serikali inadhamiria kujenga na kuendelea na ujenzi huo kwenye Wilaya zisizo na Magereza ikiwemo Wilaya ya Chunya kadri ya hali ya Bajeti itakavyoruhusu.