Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 12 2019-04-03

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (Kn.y. MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:-

Ukarabati wa Kituo cha Afya Mbwera yakiwemo majengo ya upasuaji, Wodi ya Wazazi na mengineyo unakwenda kwa kasi sana:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka umeme kwenye Kituo cha Afya Mbwera?

(b) Je, ni lini kazi hiyo itaanza?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Kibiti, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Mbuchi, Mbwera Mashariki na Mbwera Magharibi kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA) III unaoendelea. Kazi hiyo itaanza Mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021. Mradi huo unahusisha kupeleka umeme wa Gridi ya Taifa katika eneo la Mbwera kutoka Muhoro kwa kujenga njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 40; ujenzi wa njia ya kusambaza umeme yenye urefu wa kilomira 2.78; ufungaji wa transfoma moja (1) ya KVA 50; pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 48 ikiwemo Kituo cha Afya cha Mbwera. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 1.56. Ahsante.