Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 1 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 7 2019-04-02

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Katika kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu na nchi jirani ya Kenya, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) limechukua mashamba ya baadhi ya wananchi wa Kata ya Mwakijembe:-

Je, ni lini wananchi hao watapewa fidia kwa ajili ya ardhi/mashamba yao yaliyochukuliwa na Jeshi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limeanzisha Kituo cha Ulinzi katika eneo la Kata ya Mwakijembe, Wilaya ya Mkinga lenye hekari moja mwaka 2017. Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga iliona umuhimu wa kutenga eneo hilo kwa matumizi ya Jeshi ili kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya mpakani. Eneo hilo awali lilikuwa ni shamba darasa la mradi wa umwagiliaji uliokuwa unaendeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa eneo hili lilikuwa linasimamiwa na uongozi wa Wilaya kabla ya Jeshi kuingia hapo, ni busara suala la fidia kama lipo likawasilishwa kwenye uongozi wa Wilaya ya Mkinga.