Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 10 Industries and Trade Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 119 2019-02-08

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:-

(a) Je, ni viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda?

(b) Je ni viwanda vingapi vilibinafsishwa na kushindwa kuendelezwa ambavyo vimerejeshwa Serikalini tangu kuanza utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda?

(c) Je sekta ya viwanda inachangia kiasi gani pato la Taifa?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali na Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbageni, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na juhudi za kujenga uchumi wa viwanda zinazofanywa na Serikali ya Awamu Tano, tangu iingie madarakani hadi kufikia Disemba, 2018 jumla ya viwanda 3,504 vimeanzishwa nchini. Viwanda hivyo vinajumuisha viwanda vidogo sana 2,500; viwanda vidogo 943; viwanda vya kati 51; na viwanda vikubwa 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikifanya tathmini ya viwanda 156 vilivyobinafsishwa na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukulia kwa viwanda 68 ambavyo havijaendelezwa. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilijiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na kuiwezesha Ofisi ya Msajili wa Hazina kuchukua hatua. Kutokana na kuchukua hatua hiyo tayari viwanda 14 vimesharejeshwa Serikalini na juhudi za kuvitafutia wawekezaji wengine walio tayari kuviendeleza zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa hali ya uchumi ya mwaka 2017, mchango wa sekta ya viwanda katika pato la Taifa ni asilimia 5.5, ikilingalishwa na asilimia 4.9 ya mwaka 2016, sawa na ongezeko la asilimia 0.6.