Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 8 Industries and Trade Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 98 2019-02-06

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA aliuliza:-

Seikali ina mkakati gani wa kujenga Kiwanda cha Kusindika Nyanya katika maeneo ya Mto Ngarenanyuki?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kufanya marekebisho kidogo ya Kiswahili sanifu kwenye majibu yangu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Stephen Lemomo Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua kuwa eneo la Mto Ngarenanyuki katika Wilaya za Arumeru na Longido ni miongoni mwa maeneo yanayolimwa nyanya kwa wingi nchini. Ndiyo maana kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo tumeendelea kuweka mazingira wezeshi sambamba na kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya kusindika nyanya. Kwa kuwa ni muhimu kwa kiwanda kuwa na uhakika wa malighafi za kutosha mwaka mzima namwomba Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kuhamasisha uzalishaji zaidi wa nyanya ikiwezekana zipatikane kwa mwaka mzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupita SIDO imekuwa ikitoa mafunzo ya aina mbalimbali kuhusu ujasiriamali na usindikaji wa mazao ya kilimo. Naomba wananchi wa eneo wa Mto Ngarenanyuki katika Wilaya hizo mbili na Wilaya nyingine nchini waitumie fursa hiyo kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kusindika mazao ikiwemo nyanya.