Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Madini 93 2019-02-06

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:-

Wakazi wa Kitongoji cha Mafulungu kilichopo katika Kijiji cha Ilangali, Kata ya Manda wanajishuhgulisha na uchimbaji wa madini.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wakazi hao ili shughuli zao za uchimbaji ziwe za ufanisi na zenye tija?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata ya Manda, Kijiji cha Ilangali, Kitongoji cha Mafulungu, Wizara ilishatoa leseni 16 za wachimbaji wadogo wa madini ya jasi (gypsum) zilizotolewa kuanzia mwaka 2014 hadi 2016. Hadi sasa Tume ya Madini imepokea maombi 32 ya leseni za uchimbaji mdogo wa madini ya jasi kutoka katika eneo hilo. Maombi 16 yapo katika hatua za mwisho za kutolewa leseni na maombi 16 bado hayajakamilisha vigezo vya kupatiwa leseni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuwahamasisha wakazi wa Mafulungu kujishughulisha na uchimbaji wa madini sambamba na kutunza kumbukumbu za uzalishaji na mauzo ili waweze kuaminika na kukopeshwa na taasisi za fedha. Aidha, nawashauri wachangamkie fursa ya uwepo wa madini hayo katika kitongoji chao kwani mahitaji yake ni makubwa hasa katika viwanda vya saruji nchini na nchi za nje baada ya Serikali kuzuia uingizaji wa madini hayo kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Madini inaendelea kutoa elimu kwa wamiliki wa leseni kuhusu uchimbaji bora wa madini ya jasi na kuwataka kuchangia miradi ya maendeleo katika jamii kwenye maeneo yanayowazunguka katika migodi yaani kwa maana ya Corporate Social Responsibility kwani ni takwa la kisheria kama inavyoelekezwa katika kifungu cha 105 cha Sheria ya Madini ya mwaka 2010 kama ilivyorekebishwa mwaka 2017.