Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 14 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Maji na Umwagiliaji | 63 | 2019-02-04 |
Name
Richard Phillip Mbogo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nsimbo
Primary Question
MHE. RICHARD P. MBOGO aliuliza:-
Upatikanaji wa maji safi na salama katika Jimbo la Nsimbo ni asilimia 40 chini ya wastani wa kitaifa vijijini wa asilimia 61.1 ili kufikia wastani huo inahitajika fedha kiasi cha bilioni 15:-
Je, Serikali ipo tayari kuitengea Halmashauri ya Nsimbo angalau bilioni tatu kila mwaka wa fedha?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Philip Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, kama ifuatvyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2018/2019 imeitengea Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo kisi cha shilingi bilioni 1.413 ikiwa ni fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji inayoendelea kutelezwa katika vijiji vya Sitalike, Igongwe, Itenka, Nduwi pamoja na ufungaji wa pampu za mkono katika vijiji vya Kashelami, Kapanda, Wenyeji, Imilamate, Kambuzi Halt, Ofisi ya DED - Nsimbo, Katambike, Kabuga, Kituo cha Afya Katumba, Buremo, Ikondamoyo na Ndurumo A.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wote wananufaika na huduma ya maji wakiwemo wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Serikali imejiwekea lengo la kuhakikisha huduma ya maji inafikia asilimia 85 upande wa maji vijijini na asilimia 95 miji ya mikoa ifikapo 2020. Hivyo, Serikali itaendelea kutenga fedha mwaka hadi mwaka kwa ajili ya utekelezaji wa miradi maji nchi kote ili kuweza kufikia malengo hayo.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved