Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 14 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Maji na Umwagiliaji | 62 | 2019-02-04 |
Name
Julius Kalanga Laizer
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Monduli
Primary Question
MHE. JULIUS K. LAIZER aliuliza:-
Tatizo la maji Jimbo la Monduli limeongeze kwa sasa baada ya Mabwawa zaidi ya 43 kati ya 51 kujaa tope na mengine kupasuka:-
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa muda mfupi na muda mrefu wa kuwapatia maji wananchi wa Esilalei, Makuyuni, Mswakini na Ohukai kabla ya mwaka 2020?
(b) Mradi wa maji ya kisima cha Ngaramtoni umefika katika Kata ya Monduli Mjini na Engutoto; je, ni lini Serikali itasambaza maji kwa wananchi wa Vijiji vya Lashaine, Ar Katan na Meserani chini?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Julius Kalanga Laizer, Mbunge wa Monduli, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuwapatia maji wananchi wa Esilalei Makuyuni, Mswakini na Otukai kabla ya mwaka 2020 Serikali imekuwa ikijenga mabwawa ya kuhifadhi maji katika Wilaya ya Monduli kutokana na Wilaya hiyo kukosa vyanzo vya uhakika vya maji kama vile chemchem na vyanzo vya maji chini ya ardhi. Kwa upande wa Vijiji vya Makuyuni na Mswakini vinapata maji kupitia visima virefu vilivyochimbwa kwenye vijiji hivyo na vijiji vya Esilalei na Otukai vinapata maji kupitia vyanzo vya Bwawa ya Otukai, Esilalei na JKT Makuyuni.
Mheshimiwa Spika, mwaka 2017/2018 Serikali ilitekeleza mradi wa maji wa Ngaramtoni ambapo awamu ya kwanza ilihusisha huduma ya usambazaji katika kijiji cha Meserani Juu. Awamu ya pili itahusisha usambazaji wa maji katika Kijiji cha cha Meserani Chini na kazi hiyo inategemea kuanza mwezi Julai, 2019. Kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Monduli imetengewa jumla ya shilingi bilioni
1.2 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji. Serikali itaendelea kutenga fedha na kutoa fedha ili kuhakikisha hadi kufikia mwaka 2020 vijiji vyote vya Arktana, Nanja, Esilalei, Makuyuni, Mswakini, Otukai na Mti Mmoja vimepatiwa huduma ya maji.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved