Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 14 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 57 | 2019-02-04 |
Name
Halima James Mdee
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE) aliuliza:-
Mwezi Novemba, 2018, Rais aliutangaza ulimwengu kwamba Serikali yake itanunua korosho zote kwa bei isiyopungua shilingi 3,000/= kwa kilo.
(a) Je, mpaka sasa ni kiasi gani kimetumika na kimetoa chanzo kipi na je, tani ngapi zimenunuliwa?
(b) Je, Wakulima/Vyama vya Msingi vingapi vimelipwa na vingapi bado havijalipwa?
(c) Je, zoezi hilo linatarajiwa kukamilika lini?
Name
Omary Tebweta Mgumba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini Mashariki
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Jimbo la Kawe lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, makadirio ya uzalishaji wa korosho msimu wa 2018/2019 ni zaidi ya tani 240,000 za korosho ghafi. Hadi kufikia tarehe tarehe 30 Januari, 2019, Serikali imekusanya jumla ya tani 214,269.684 za korosho ghafi zenye thamani ya Sh.707,089,957,200 sawa na asilimia 89.3 ya lengo la uzalishaji.
Mheshimiwa Spika, ununuzi wa korosho unafanywa na Taasisi ya Serikali ya Bodi ya Nafaka na mazao mchanganyiko ambapo malipo yaliyolipwa na kuingizwa kwenye akaunti za wakulima hadi tarehe 30 Januari, 2019 ni kiasi cha Sh.424,849,405,110 zilizotokana na korosho za wakulima kiasi cha tani 134,535,904. Aidha Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko ni Taasisi ya kibiashara yenye lengo la kupata faida na mtaji wake unatokana na ruzuku kutoka Serikali na mikopo kutoka Taasisi kama Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), NMB, CRDB na Benki zinginezo.
(b) Mheshimiwa Spika, jumla ya wakulima laki 390,466 wamekwishalipwa hadi kufikia tarehe 30 Januari 2019. Aidha Vyama vya Msingi 603 vimelipwa kati ya Vyama vya Msingi 605 vilivyohakikiwa.
(c) Mheshimiwa Spika, zoezi la operesheni korosho linaendelea vizuri na linatarajia kukamilika ifikapo tarehe 15 Februari, 2019.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved