Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 14 | Sitting 6 | Industries and Trade | Viwanda na Biashara | 56 | 2019-02-04 |
Name
Ajali Rashid Akibar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Newala Vijijini
Primary Question
MHE. AJALI R. AKBAR aliuliza:-
Wananchi wa Mtwara ni wakulima wakubwa wa zao la muhogo:-
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia masoko ya uhakika wakulima hao?
(b) Je, kwa nini Serikali isiwapatie wajasiriamali, hasa akina mama, viwanda vya kuchakata muhogo?
Name
Eng. Stella Martin Manyanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nyasa
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ajali Rashid Akbar, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, zao la muhogo ni miongoni mwa mazao ambayo Wizara yangu imepanga kuyapa msukumo wa kuyaongezea thamani ili yaweze kuchangia katika ukuzaji wa uchumi na kuongeza pato ya Taifa. Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imekuwa na mkakati mbalimbali wa kuliongezea thamani na kupanua wigo wa soko la zao la muhogo. Itakumbukwa kuwa mnamo tarehe 28 Juni, mwaka 2018 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa aliagiza Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo kuunda Kamati Maalum ya Wataalam na kupitia changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima na kushindwa kuuliza zao hili katika soko la China. Kamati imeshakamilisha kazi yake na imeshatoa mapendekezo yake Serikalini kwa ajili ya utekelezaji.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa kiwanda cha Cassava Starch of Tanzania Corporation kilichopo Mbalala Mkoa wa Lindi chenye uwezo wa kuchakata tani 60 za muhogo kwa siku umekamilika kwa asilimia 90. Kiwanda hiki kimeanza uzalishaji wa unga wa muhogo kwa majaribio mwezi Januari, 2019. Kukamilika kuanza uzalishaji rasmi katika kiwanda hiki kutatoa fursa ya soko kwa wakulima wa muhogo wa Mikoa ya Kusini. Vilevile kutokana na kukua kwa soko la unga wa muhogo duniani nawahimiza wajasiriamali kupata ushauri kutoka kwa wataalam wakiwemo SIDO na TIRDO kwa lengo la kuelimishwa namna bora kuchakata zao hili ili kuuza katika masoko hayo hususan China ambako mahitaji ya muhogo ni makubwa.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved