Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 52 2019-02-01

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:-

Jimbo la Mikumi linaitwa Jimbo la giza kutokana na kata zake nyingi kutokuwa na umeme, kama Kata ya Ulaya, Zombo, Tindiga, Mhenda, Kilangali, Vidunda na kadhalika:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Jimbo hilo ambalo limebarikiwa kuwa na Mbuga za Wanyama na vivutio kadha wa kadha?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mikumi lina vijiji 57, kati ya vijiji hivyo vijiji 16 vina umeme. Katika utekelezaji wa azma ya Serikali ya kufikisha umeme katika vijiji vyote nchini ifikapo mwaka 2021, vijiji 41 ambavyo havijafikiwa na umeme katika Jimbo la Mikumi vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu unaoendelea sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Mikumi kwa sasa inafanyika katika vijiji nane vya Ihombwe, Kwalukwambe, Vidunda, Madizini, Zombolumbo, Malui, Udung’hu na Kigunga. Kazi za kupeleka umeme katika vijiji hivyo vinahusisha ujenzi wa kilomita 26 za njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 na kilometa 32 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4, ufungaji wa transfoma 16 na kuunganishia umeme wateja wa awali 533 na gharama za mradi ni shilingi bilioni mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi wa REA Awamu ya Tatu, mzunguko wa kwanza katika Jimbo la Mikumi pamoja na Mkoa wa Morogoro kwa ujumla ulianza mwezi Julai, 2018 ambapo Kampuni ya State Grid Electical and Technical Works Ltd. inatarajia kukamilisha kazi hizo mwezi Juni, 2019. Vijiji vilivyobaki 33 vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu unaotarajiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2020/2021.