Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 49 2019-02-01

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:-

Kuna harufu mbaya inayotoka kwenye chumba cha Mahabusu katika Kituo cha Polisi Mazizini Zanzibar na kuwa kero kwa Askari na wananchi wanaofika kupata huduma kituoni hapo.

Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati kituo hicho ili kuondoa harufu hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bi. Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa hali ya jengo la Kituo cha Polisi Mazizini hairidhishi. Kwa kutambua hilo, Serikali ikishirikiana na wadau wa usalama inaendelea na ujenzi wa Kituo kipya cha Polisi cha kisasa katika eneo la Chukwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, jengo hili jipya lipo katika hatua za mwisho za umaliziaji na mara ujenzi utakapokuwa umekamilika shughuli za kiusalama za Jeshi la Polisi za Kituo Kikuu cha Wilaya ya Magharibi ‘B’ katika Mkoa wa Mjini Magharibi zitahamishiwa kutoka Kituo cha Mazizini na kwenda Chukwani.