Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 38 2019-02-01

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:-

Vigezo vilivyotumika kuchagua Vituo vya Afya 100 kupatiwa shilingi milioni 700 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maabara na upasuaji wa akina mama wanaojifungua kwa maana ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya maabara na upasuaji na shilingi milioni3 00 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa toka MSD ni vigezo ambavyo pia vipo katika Vituo vya Afya Duthumi, Tawa, Mvula na Mtamba katika Jimbo la Morogoo Kusini.

Je, ni lini Seikali itawatendea haki wananchi wa Morogoro Kusini kwa kuwatengea fedha ili kukamilisha miundombinu ya upasuaji angalau kituo kimoja Kata ya Duthumi, Tawala Mvuha na Mtamba?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, Mbunge wa Morogoro Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza Mpango wa Kuboresha Vituo vya Afya nchini ambapo hadi sasa Vituo vya Afya 350 vimepatiwa fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati.

Mheshimiwa Naibu Spika, vigezo vilivyotumika kuchagua vituo hivyo vinavyokarabatiwa na kujengwa ni uhitaji mkubwa wa huduma za dharura na upasuaji kwa mama wajawazito, sababu za kijiografia na umbali mrefu ambao wananchi wanatembea kupata huduma za dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali ilitoa kiasi cha shilingi million 500 kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa Kituo cha Afya cha Duthumi kilichopo katika Jimbo la Morogoro Kusini. Vilevile katika mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilion1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro inayojengwa katika Makao Makuu ya Halmashauri eneo la Mvuha.