Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 25 2019-01-30

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-

Serikali iliahidi kuanza utekelezaji wa mradi wa umeme wa ujazo (Densification) Mkoani Geita kuanzia mwezi Oktoba, 2018 lakini hadi sasa mradi huo haujaanza:-

Je, ni lini mradi huo utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Mbogwe?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya tatu ya mradi kabambe ya kusambaza umeme vijijini unahusisha mradi wa ujazilizi (Densification) kwa kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji ambavyo vimeshafikishiwa umeme lakini baadhi ya Vitongoji havijafikiwa na umeme. Mradi wa Grid Extension unahusu kupeleka umeme katika vijiji ambavyo havijafikiwa na miundombinu ya umeme na mradi wa Off- Grid electrification wa kuendeleza na kusambaza nishati jadidifu katika maeneo yaliyo mbali na Grid ikiwa ni pamoja na visiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilikamilisha kupeleka umeme katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi wa ujazilizi mwezi Septemba, 2018 katika awamu hiyo Vijiji na Vitongoji 305 vya Mikoa ya Arusha, Iringa, Mara, Mbeya, Njomba, Pwani, Tanga na Songwe ambapo jumla ya wateja 29,950 wameunganishiwa umeme na gharama ya mradi ilikuwa ni shilingi bilioni 68.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya pili ya mradi ya ujazilizi utapeleka umeme katika mikoa 26 Tanzania Bara katika Vitongoji 1,103 vikiwemo Vitongoji vya Wilaya ya Mbogwe kwa kuunganishia umeme wateja wa awali 69,079. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 197.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi utaanza mwezi Machi, 2019 kwa muda wa miezi 12.