Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 2 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 23 2019-01-30

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA (K.n.y. MHE. JOHN J. MNYIKA) aliuliza:-

Ili kuharakisha upimaji na urasimishaji wa ardhi na makazi, Serikali iliruhusu kampuni binafsi kufanya kazi hiyo katika maeneo mbalimbali.

(a) Je, ni lini kampuni zinazofanya kazi hiyo zitatoa hati za ardhi au leseni za makazi kwa wananchi?

(b) Je, ni vikwazo gani vinakabili zoezi hilo na Serikali inachukua hatua gani kuviondoa ili kuzisaidia kampuni hizo kumaliza kazi hiyo kwa haraka?

(c) Je, ni lini Serikali itakamilisha mpango kabambe (masterplan) mpya ya Jiji la Dar es Salaam ili uwe dira katika upangaji, upimaji na urasimishaji?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Mnyika, Mbunge wa Kibamba, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, umilikishwaji wa ardhi hufanywa kwa mujibu wa Sheria Na.4 ya mwaka 1999 ambayo inampa Kamishna wa Ardhi mamlaka ya kutoa hati au leseni za makazi. Hivyo, lengo la kusajili makampuni ya upangaji na upimaji ardhi ni kuongeza kasi ya upangaji na kupima ardhi nchini lakini hati miliki za ardhi hiyo hutolewa na Kamishna baada ya mwananchi kulipa gharama za umilikishaji zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kimingi kwa sasa hatuna kikwazo au vikwazo vinavyokabili zoezi la urasimishaji ardhi nchini zaidi ya changamoto ya mwitikio mdogo wa wananchi katika maeneo mbalimbali. Awali zoezi hili lilikuwa linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ramani za msingi (base maps), uhaba wa vifaa vya kisasa vya upimaji, matumizi ya teknolojia duni, baadhi ya wananchi kutokuwa tayari kulipia gharama ya ardhi kwa ajili ya miundombinu na uelewa mdogo kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuondoa changamoto hizo, Serikali iliweka mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa picha za anga katika Jiji la Dar es Salaam na KIbaha na kuandaa ramani za msingi (base maps) mpya za mwaka 2016, ununuzi wa vifaa vya kisasa vya upimaji, kuongeza mtandao wa alama za msingi za upimaji yaani control points, usimikaji wa mfumo wa ILMIS kwa ajili ya kurahisisha umilikishaji na uhamasishaji wa wananchi kuhusu zoezi la urasimishaji.

(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, rasimu ya mwisho ya mpango kabambe ya Jiji la Dar es Salaam imekamilika na nakala za kielektroniki za rasimu hiyo zimesambazwa kwa wadau kwa ajili ya kupitia na kutoa maoni yao. Aidha, rasimu ya mpango huo imewekwa kwenye tovuti ya Wizara www.lands.go.tz ili kwezesha wadau kutoa maoni yao. Kwa sasa Mtaalam Mwelekezi anafanya mawasilisho ya rasimu hiyo katika mikutano ya hadhara (public hearing) katika Mamlaka zote za Upangaji za Jiji la Dar es Salaam ili kuapata maoni ya wananchi.