Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 10 2019-01-29

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-

Zao la Korosho pamoja na kuingiza mapato makubwa Serikalini bado lina changamoto nyingi sana katika uuzaji wake kwa upande wa Wakulima:-

Je, Serikali ipo tayari kuondoa changamoto hizo ili kuleta tija kwa Wakulima?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maftah Abdallah Nachuma Mbunge wa Jimbo la Mtwara mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli zao la Korosho ni mojawapo ya mazao ya Kilimo yanayoliingizia Taifa mapato ambapo katika kipindi kilichoishia Oktoba, 2018, zao la Korosho liliingizia Taifa fedha za kigeni za Kimarekani zaidi ya dola milioni mia tano sabini na tano pointi sita sawa na zaidi fedha za Kitanzania trilioni moja nukta tatu ikilinganishwa na mazao mengine ya biashara. Aidha, pamoja na mchango wa zao hilo katika uchumi wa Taifa, zao la Korosho limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali ambapo Serikali imekuwa ikizitafutia ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, changamoto hizo ni pamoja na kuyumba kwa bei ya zao la Korosho katika soko la dunia kutokana na Korosho kuuzwa ikiwa ghafi bila kuongezewa thamani; Tija ndogo katika uzalishaji wa wakulima; baadhi ya wakulima kutotumia miche bora na matumizi hafifu ya pembejeo ikiwemo viuadudu kama sulphur; wakulima kutozingatia Kanuni bora za Kilimo katika uzalishaji, uvunaji na uhifadhi hafifu wa Korosho; uwezo mdogo wa maghala ya kuhifadhia Korosho na baadhi ya wakulima kuchanganya Korosho na mawe na mchanga kwa ajili ya kuongeza uzito wakati wa mavuno ambao unashushia ubora.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hizo, Serikali imeboresha mfumo wa uuzaji wa Korosho kwa kuimarisha usimamizi na ukaguzi kuanzia ngazi ya vyama vya msingi, maghala makuu, maghala ya hifadhi na kutoa elimu kwa wakulima; kurejesha Kiwanda cha BUCCO cha Mkoani Lindi cha kubangua Korosho ujenzi wa maghala matatu ya kuhifadhia Korosho katika Mikoa ya Ruvuma, Pwani na Tanga ili kuongeza Kiwango cha kuhifadhi na ubora wa Korosho pamoja na kuzalisha miche bora zaidi ya milioni kumi na kuisambaza kwa wakulima.

Mheshimiwa Spika, mikakati mingine ni pamoja na kuimarisha mnyororo wa thamani katika zao la Korosho ili kuongeza uzalishaji, kuimarisha usambazaji wa pembejeo za Kilimo kwa wakati, kutoa huduma za ugani pamoja na kuweka mazingira wezeshi na kuwajengea uwezo wabanguaji wa ndani wa Korosho kwa lengo la kuongeza thamani ya Korosho inayozalishwa nchini.