Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 session 13 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 03 2018-11-06

Name

Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA aliuliza:-
Sera ya Serikali ni kuwa na Hospitali za Wilaya na Vituo vya Afya katika kila Kata:-
• Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko?
• Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya katika Kata za Kiziguzigu, Kasanda, Gwarama, Rugenge, Nyamutukiza na Kata nyingine ambazo hazina Vituo vya Afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Christopher Kajoro Chiza, Mbunge wa Buyungu, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hatua za awali za kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko zimeanza ambapo limetengwa eneo lenye ukubwa wa ekari 32 katika Mtaa wa Kanyamfisi karibu na yanapojengwa Makao Makuu ya Wilaya.
Mheshimiwa Spika, Serikali inajenga Hospitali za Wilaya kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza zimetengwa shilingi bilioni 100.5 kuanza ujenzi wa Hospitali 67 za Wilaya. Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko itapewa kipaumbele cha kujenga Hospitali ya Wilaya katika awamu inayofuata.
Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa shilingi bilioni 4.2 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo tisa vya afya katika Mkoa wa Kigoma. Kati ya fedha hizo, halmashauri ya Wilaya ya Kakonko imetengewa Sh.500,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Gwanumpu. Maeneo yaliyobaki zikiwemo Kata za Kizuguzugu, Kasanda, Rugenge, Gwarama na Nyamtukuza yatapewa kipaumbele kulingana na upatikanaji wa fedha.