Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 22 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 180 2018-05-04

Name

Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. RASHID ALI ABDALLAH aliuliza:-
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kama vile LAPF, PSPF, PPF, NSSF na NHIF imesaidia sana kutoa mikopo hasa kwa Serikali kwa ajili ya maendeleo ya jamii:-
Je, Serikali imefanya juhudi gani kurejesha mikopo hiyo kwa wakati?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Ali Abdallah, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 Serikali ilifanya uhakiki wa deni la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii linalotokana na mikopo ya uwekezaji kwenye miradi mbalimbali ili kuandaa utaratibu wa malipo. Jumla ya deni lililowasilishwa Serikalini kwa ajili ya uhakiki kwa mifuko yote ni shilingi trilioni 2.1 na deni lililokubalika baada ya uhakiki ni shilingi trilioni 1.2.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya uhakiki kukamilika, Serikali ilianza kuandaa utaratibu wa kulipa deni hilo kwa kutumia hati fungani maalum zilizotarajiwa kuiva ndani ya kipindi cha kati ya miaka mitatu (3) na 20. Hata hivyo, wakati zoezi la kuandaa hati fungani likiendelea, Serikali ilipendekeza na Bunge lako Tukufu kuridhia mapendekezo ya Serikali ya kuunganisha Mifuko ya Pensheni na kuunda Mifuko miwili mmoja kwa ajili ya sekta ya umma na mwingine kwa ajili ya sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua hiyo, ilisababisha Serikali kusitisha zoezi la kuandaa na kutoa hati fungani maalum hadi hapo taratibu za kuunganisha Mifuko ya Pensheni zitakapokamilika.