Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 179 2018-05-04

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:-
Jimbo la Kigoma Kusini lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,178 lina jiografia mbaya na idadi ya wakazi wake ni kubwa sana:-
a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuligawa jimbo hilo na kuanzisha halmashauri nyingine ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za kijamii kiurahisi?
b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo katika Tarafa ya Nguruka?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali refu la Mheshimiwa Hasna Sudi Katundu Mwilima, Mbunge wa Kigoma Kusini, lenye vipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-
• Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Ibara ya 75 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imepewa mamlaka ya kuyagawa majimbo ya uchaguzi kwa kuzingatia vigezo vya idadi ya watu, jiografia, hali ya mawasiliano, ukubwa wa jimbo na uwezo wa ukumbi wa Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili Jimbo lolote ligawanywe, Tume hutoa tangazo kuhusu nia hiyo. Baada ya tangazo, mapendekezo hujadiliwa katika vikao vya Halmashauri, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa na hatimaye kuwasilishwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo hutangaza jimbo jipya baada ya kupata kibali cha Rais.
• Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo vinavyozingatiwa katika kuanzisha Mamlaka za Miji Midogo ni pamoja na idadi ya watu wasiopungua elfu hamsini, kata zisizopungua tatu, eneo lisilopungua kilomita za mraba mia moja na hamsini, viwanja vilivyopimwa visipungue asilimia
30 ya eneo lote, uwepo wa mpango kabambe wa uendelezaji wa mji (master plan) na huduma za jamii za kukidhi ukuaji wa mji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, mapendekezo ya kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo yanapaswa kuanzia kwenye Mkutano Mkuu wa Kijiji, Kamati ya Maendeleo ya Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa kwa kuzingatia vigezo hivyo kwa mujibu wa sheria. Mapendekezo ya vikao hivyo huwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kumshauri ipasavyo Waziri mwenye dhamana.