Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 479 2018-06-25

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-
Katika kampeni za uchaguzi mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga Kituo cha Afya katika Mji wa Nalasi na kutoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya
Mchoteka:-
(a) Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nalasi?
(b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mchoteka?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Afya - Nalasi ulianza Oktoba, 2013 kwa gharama ya shilingi milioni 80 ambapo awamu ya kwanza ilihusisha ujenzi wa msingi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD). Katika mwaka wa fedha 2017/2018, kiasi cha shilingi milioni 75 zimetengwa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa hicho kituo cha afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka kipaumbele na kutoa shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya nane katika Mkoa wa Ruvuma ambapo kati ya hivyo, vituo vya afya viwili vinajengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ambavyo ni Msakale kilichogharimu shilingi milioni 400 na Kituo cha Afya Matemanga kilichogharimu shilingi milioni 500.
(b) Mheshimwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina gari moja ambalo linahudumia vituo vyote vya afya kikiwemo Kituo cha Afya Mchoteka. Hata hivyo, gari hiyo kwa sasa ni chakavu kwa kuwa ilinunuliwa tangu mwaka 2007. Halmashauri inashauriwa kuweka kipaumbele na kutenga fedha katika mwaka wa fedha 2019/2020 kwa ajili ya ununuzi wa gari lingine la wagonjwa.