Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 56 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 473 2018-06-22

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSSA R. NTIMIZI aliuliza:-
Wananchi Halmashauri ya Wilaya ya Tabora kwa kushirikiana na Mbunge wamejenga kituo kikubwa cha Polisi katika Kata ya Loya kilichogharimu zaidi ya Sh.100,000,000/= lakini mpaka sasa hakijaanza kufanya kazi:-
• Je, Serikali ipo tayari kutenga bajeti kusaidia ujenzi wa nyumba za askari na kurekebisha upungufu mbalimbali uliopo?
• Je, Serikali ipo tayari kutoa gari jipya ili kusaidia kurahisisha kazi ya Ulinzi na Usalama katika eneo hilo kwani kituo hicho kipo kilomita 120 kutoka Makao Makuu ya Wilaya – Isikizya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Igalula, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itatenga fedha kwa ajili ya kumaliza Kituo cha Polisi cha Kata ya Loya ambapo nyumba, chumba cha kuhifadhi Mahabusu na chumba cha kuhifadhi silaha vitaimarishwa ili kituo hicho kianze kutoa huduma kwa wananchi. Aidha, napenda kutoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Wananchi pamoja na Mheshimiwa Mbunge kwa kufanikisha ujenzi wa kituo hicho cha Polisi katika Kata ya Loya.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Uyui ambayo Makao Makuu yake yapo Kata ya Isikizya ina magari matatu na moja ni bovu ambalo linahitaji matengenezo. Serikali inaendelea na mchakato wa kutafuta magari kwa ajili ya Jeshi la Polisi na pindi yatakapopatikana yatagawiwa katika maeneo mbalimbali yenye mahitaji nchi nzima.