Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 458 2018-06-20

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:-
Kituo cha Afya Mlandizi kimetimiza vigezo vyote vya kuwa Haspitali ya Wilaya:-
Je, ni lini sasa Serikali itapandisha hadhi Kituo hicho kuwa Hospitali ya Wilaya?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Malandizi bado hakijakidhi vigezo vya kukifanya kiwe Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, Serikali haina mpango wa kukipandisha hadhi Kituo hicho kuwa Hospitali ya Wilaya. Serikali imeamua Kituo hicho kiendelee kutoa huduma kama Kituo cha Afya. Hata hivyo, Serikali iliiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha itenge eneo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali Wilaya.
Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeshatenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika mwaka wa 2018/2019 kwa ajili ya ujenzi huo. Pia Halmashauri imeshatenga eneo la ekari 32 lililopo katika Kitongoji cha Disunyala, zamani lilikuwa shamba la United Farming Cooperation kwa ajili ya ujenzi huo.