Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 52 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 443 2018-06-18

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA M. MLATA (K.n.y. MHE. AISHAROSE N. MATEMBE) aliuliza:-
Sanaa ya Maigizo na muziki ni miongoni mwa Sekta zinazochangia asilimia kubwa ya vijana kujiajiri lakini kuna Vyuo vichache nchini vinavyotoa elimu hiyo ya sanaa ya muziki na maigizo ambavyo ni Chuo cha Sanaa Bagamoyo na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam huku masharti yake yakiwa ni changamoto kwa vijana wa mikoani:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha matawi ya Vyuo hivyo kwenye Kanda ama Mikoa ili kuongeza fursa zaidi kwa vijana?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Ndogholi Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mafunzo ya Elimu ya Sanaa ya Maigizo na Muziki au kwa ujumla Sanaa, yanatolewa kwa ngazi ya Shahada na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Dodoma na Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam kwa upande wa Serikali na Chuo Kikuu cha Tumaini Arusha kwa upande sekta binafsi. Aidha, mafunzo kwa ngazi ya Stashahada na Cheti kwa Vyuo vya Serikali hutolewa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yenye matawi takribani nchi nzima. Vipo vilevile vyuo binafsi ambavyo hutoa mafunzo ngazi ya Stashahada pamoja na Cheti.
Mheshimiwa Spika, nitoe rai kwa vijana na wadau wengine wanaotaka kubobea kwenye sanaa wajiunge na vyuo hivi ambavyo vimetawanyika nchi nzima. Aidha, nawapongeza wadau wote walioanzisha vyuo hivyo ili kuunga mkono jitihada za Serikali.