Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 49 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 417 2018-06-12

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU (K.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA) aliuliza:-
Serikali ilianzisha Wakala wa Misitu (TFS) kwa lengo la kuhifadhi misitu, kulinda na kusimamia matumizi endelevu ya rasilimali ya misitu:-
Je, ni kwa kiasi gani Maafisa wa Misitu walioko Mikoani, Wilayani wameweza kuokoa misitu inayozidi kuteketea hapa nchini?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, Mbunge wa Kaliua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania (TFS) inasimamia misitu ya hifadhi ya Serikali Kuu ipatayo 455 sawa na hekta15.48 milioni ambayo ni takriban asilimia 35 ya eneo lote la misitu nchini. Eneo hili hujumuisha misitu ya asili na ile ya kupandwa (Forest Plantations). Aidha, TAMISEMI wanasimamia hifadhi 161 sawa na hekta 3.36 milioni wakati serikali za vijiji zinasimamia hifadhi za misitu 1,200 sawa na hekta milioni 21.6. TFS ina kazi za kutafiti, kuhifadhi, kulinda na kusimamia matumizi endelevu ya misitu yote nchini. Kazi hizi zinatekelezwa na Maafisa Misitu wa TFS waliopo katika Kanda Saba na Wilaya 135 za Tanzania Bara wakishirikiana na Maafisa Misitu waliopo chini ya Halmashauri za Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa Misitu walioko Mikoani na Wilayani wameweza kusimamia hifadhi za misitu hii na kuwezesha kurejea kwa uoto wa asili katika misitu 271 nchini. Kazi zilizotekelezwa na Maafisa hao ni pamoja na soroveya (Survey and Resurvey) ya misitu husika; kuimarisha mipaka ya misitu kwa kuwezesha takriban kilomita 13,100 za mipaka hii kusafishwa; Kuweka vingingi (beacons) 14,200 vyenye kuonyesha mipaka na hifadhi; Kupanda miti katika mipaka ya misitu na kuweka mabango (sign boards) 4,553 kwa ajili ya kutoa taarifa za uwepo wa misitu ya hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Maafisa Misitu wameendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu hatari ya kuwasha moto katika misitu ya hifadhi, athari za kilimo cha kuhamahama, ufugaji ndani ya hifadhi, uchimbaji wa madini na utengenezaji wa mkaa usiozingatia weledi.