Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 49 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 415 2018-06-12

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA aliuliza:-
Kumekuwa na tatizo kubwa la ukosefu wa barabara pembezoni mwa Ziwa Nyasa, hususan Wilaya ya Ludewa na Mkoa wa Njombe; eneo hilo lenye urefu wa kilomita 150 hutegemea usafiri wa meli ambao hauna tija kwa wananchi walio wengi:-
(a) Je, Serikali itawasaidia vipi wananchi wa maeneo hayo yenye vijiji 22 kupata barabara ya uhakika?
maeneo hayo yenye vijiji 22 kupata barabara ya uhakika?
(b) Kwa kuwa wananchi wameanza kutengeneza wenyewe barabara kwa nguvu zao. Je, Serikali inatoa tamko gani la kuunga mkono juhudi hizo za wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deogratias Francis Ngalawa, Mbunge wa Ludewa, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018, TARURA imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya kufungua kipande cha barabara ya Mwambahesa - Makonde chenye urefu wa kilomita 3.67 na ujenzi wa daraja moja na box culvert mbili katika milima ya Mwambahesa. Tayari mkandarasi G.S. Contractor ameanza kupeleka vifaa katika eneo la mradi ili kuanza ujenzi ambao utakamilika Novemba, 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, TARURA Mkoa wa Njombe inaendelea na upembuzi yakinifu katika barabara yote yenye urefu wa jumla ya kilomita 115.51 ili kuifanyia matengenezo makubwa pamoja na ujenzi wa madaraja. Kazi hiyo ikikamilika itawezesha TARURA katika Mkoa wa Njombe kupata gharama halisi na kutenga fedha kwa ajili ya kufungua na kujenga barabara hizo pembezoni mwa Ziwa Nyasa.