Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 46 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 395 2018-06-07

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-
Moja ya jukumu la Serikali ni kuhudumia wafungwa kwa maana ya kukwapatia huduma za msingi kama vile chakula, mavazi na matibabu:-
Je, Serikali inafanya nini ili kuhakikisha huduma hizo za msingi katika Gereza la Kasulu zinapatikana kwani wana hali mbaya sana hasa kimavazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, huduma za wafungwa magerezani hujumuisha chakula, mavazi, matibabu pamoja na huduma nyingine muhimu ambazo hutengewa fedha katika bajeti ya Serikali ya kila mwaka. Ili kupunguza tatizo la uchakavu wa sare za wafungwa kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018, Serikali ilitenga kiasi cha shilingi milioni mia sita kwa ajili ya kushona sare za wafungwa nchi nzima. Aidha, kwa mwaka 2018/2019, Serikali imetenga shilingi milioni mia moja kwa ajili ya sare za wafungwa nchi nzima.